Jumanne 3 Februari 2026 - 10:02
Msimamo thabiti wa wahamiaji wa Afghanistan sambamba na Iran na Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu dhidi ya vitisho vya Marekani na utawala wa Kizayuni

Hawza/ Jamii ya wahamiaji wa Afghanistan wanaoishi katika Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, kupitia tamko rasmi, sambamba na kulaani vikali vitendo na vitisho vya Marekani na utawala muovu wa Kizayuni dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, imetaja makabiliano haya kuwa si ya kisiasa pekee bali ni ya kidini, na imesisitiza utayari wake kamili wa kuiunga mkono Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, katika tamko hilo, kwa kurejea asili ya kidini ya makabiliano ya Magharibi dhidi ya Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran, imesisitizwa kuwa Mapinduzi ya Kiislamu, kwa kupinga fikra ya usekula wa Magharibi katika uongozi wa dola na kuwasilisha mfano wa utawala wa Kiislamu unaojengwa juu ya kumtanguliza Mwenyezi Mungu, haki ya kijamii na ulinzi wa wanyonge—hasa katika kuunga mkono watu waliodhulumiwa wa Palestina—yamebadilisha mizania ya dunia. Wahamiaji wa Afghanistan wametaja vitisho vya hivi karibuni vya Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi kuwa ni mwendelezo wa uhalifu mpana wa kambi hii katika ardhi za Kiislamu, sambamba na kulaani waziwazi, wamesisitiza ushirikiano wa vitendo wa wahamiaji wa Afghanistan na Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu na taifa la Iran katika nyanja zote za jihadi, miqawama na ulinzi wa Uislamu Safi wa Muhammad (s.a.w.w).

Matini kamili ya tamko lililotolewa na jamii ya wahamiaji wa Afghanistan wanaoishi Iran ni kama ifuatavyo:

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu.

“Pigana nao, Mwenyezi Mungu atawaadhibu kwa mikono yenu, atawadhalilisha, atakupeni ushindi juu yao, na ataponyesha vifua vya watu waumini.”

Kama nyote mnavyojua, makabiliano ya Magharibi na Iran ya Kiislamu si ya kisiasa tu bali ni ya kidini; kwa sababu Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran yameipa changamoto fikra ya usekula wa Magharibi katika utawala na kuwasilisha utawala wa Kiislamu ambao ndani yake kumtanguliza Mwenyezi Mungu, haki, ulinzi wa wanyonge na wa Umma wa Kiislamu kumepewa nafasi ya msingi. Katika mwelekeo huu, hasa katika utetezi wa Quds na watu waliodhulumiwa wa Palestina, Mapinduzi haya yamefanya kazi ya kipekee. Sasa makabiliano ya Uislamu na ukafiri wa kimataifa yako katika hatua nyeti ya kihistoria; hivyo ni wajibu wa Waislamu wote duniani, hasa wasomi wa Umma wa Kiislamu, kuutetea Uislamu mtukufu.

Na leo, wakati Firauni wa zama hizi—baada ya mauaji ya kikatili ya mamia ya maelfu ya watu wasio na hatia na waliodhulumiwa katika ardhi za Kiislamu kuanzia Ghaza hadi Yemen, na kuanzia Afghanistan hadi Syria na Lebanon—ameilenga nguzo kuu ya hema la mhimili wa muqawama, yaani Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, na kuitishia nchi hii tukufu pamoja na Kiongozi Mkuu na Mlezi wa mambo ya Waislamu duniani kwa operesheni za kijeshi; taifa tukufu la Afghanistan, hususan jamii ya wahamiaji wa Afghanistan wanaoishi Iran, sambamba na kulaani vitisho hivi na mienendo inayokiuka maadili na sheria za kimataifa, inatangaza mambo yafuatayo:

1. Taifa tukufu la Afghanistan na wahamiaji wa Afghanistan wanaoishi Iran wanalaani vikali uingiliaji wa wazi na wa siri wa Marekani mhalifu na mbwa wake mkali—utawala muovu wa Kizayuni—na wanatangaza utayari wao wa kutoa aina yoyote ya uungaji mkono kwa mfumo wa Jamhuri ya Iran, Kiongozi mwenye hekima wa Mapinduzi, pamoja na kuokoa Mapinduzi ya Kiislamu.

2. Ndugu na dada zetu wapendwa ndani ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wafahamu kuwa, watu waumini wa Afghanistan, askari na walinzi wa heshima ya Uislamu Safi wa Muhammad (s.a.w.w) na wa heshima ya Jamhuri ya Kiislamu, wako pamoja nao katika nyanja zote za jihadi na mapambano—iwe ni ya uwanjani, ya kitamaduni, ya kisiasa au ya vyombo vya habari na ufafanuzi—na wako tayari, kama ilivyokuwa katika “vipindi vigumu na hatari vya zamani vya 

Mapinduzi ya Kiislamu,” kujitoa muhanga bega kwa bega nao na kutimiza wajibu wao.

3. Shetani Mkubwa, utawala wa Kizayuni mhalifu na wafuasi wao wote wafahamu kuwa endapo kutatokea shambulio au uchokozi wowote dhidi ya Mlezi wa mambo ya Waislamu, mbeba bendera wa heshima na uhuru wa Waislamu na watu huru duniani, na dhidi ya mfumo wa Jamhuri ya Iran, basi kambi zote na maslahi yao katika pande zote za dunia yatakuwa malengo halali ya mashambulizi ya wapiganaji wasiojulikana na vikosi vya mapambano ya Kiislamu.

Amani iwe juu ya anayefuata uongofu.

Kutoka kwa kundi la wanafunzi wa dini, wanazuoni, wapiganaji, wasomi wa vyuo vikuu na wanafunzi, wanaharakati wa kitamaduni, jumuiya za kidini, vituo vya kitamaduni, kijamii na vya habari, shule na hawza za kielimu zinazohusiana na Waafghan wanaoishi Mashhad Tukufu, Tehran, Qom, Isfahan na Shiraz.

Msimamo thabiti wa wahamiaji wa Afghanistan sambamba na Iran na Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu dhidi ya vitisho vya Marekani na utawala wa Kizayuni

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha